Thursday, January 31, 2019

JINSI YA KUPAMBANA NA AIBU MBELE YA WATU AU MTU!

JINSI YA KUPAMBANA NA AIBU MBELE YA WATU AU MTU!
Watu wenye aibu ndani yao wanafahamu fika kuwa kuna mambo mazuri yanawapita lakini wanahisi hawana jinsi ya kubadilisha hali hiyo.
Aibu kimahesabu ni sawa na:
AIBU = KUKOSA FURSA + KUKOSA FURAHA + KUFAHAMIANA NA WATU WACHACHE
Aibu ni kizuizi kikubwa sana kwa mwenye nayo kufikia mambo mazuri katika jamii.
Lakini naomba nikuambie hata kama wewe ni mmoja wao kuanzia leo
unaweza kubadilisha hali hiyo kwa kutumia hatua zifuatazo:
1.MTAZAMO WAKO JUU YA WATU WENGINE
Watu wenye aibu mara nyingi wanajaribu kujitofautisha na
watu wapya wanaokutana nao na kuwapa hadhi inayowazidi wao.
Hali hiyo itakufanya ujione huna jipya la kumueleza au kuzungumza mbele ya watu hao.
Unachopaswa kufanya ni
kumuona kila mtu mpya unayekutana naye kama wa kawaida na hana alichokuzidi na kwamba hata yeye kuna vitu hajui
au hana ambavyo wewe unavyo.
2.TAMBUA HATA WENGINE WANA AIBU PIA
Usijiweke peke yako kama ndio mtu mwenye aibu kupita wote na kwamba wengine
hawako kama wewe.
Kuanzia leo tambua kuwa kila mtu ameumbwa na aibu ndani yake pale anapokutana na mtu mpya kwahiyo ukiwa
mbele ya watu wapya
jua hata wao pia wanakuonea aibu kwa kuwa hawajui ulichonacho ni nini.
3.KUSANYA TAARIFA NYINGI KICHWANI
Mtu mwenye aibu siku zote hujiona hana chochote cha maana
kuwashirikisha wengine.
Kuna wengine wanakuwa kweli hawana vitu vya kuzungumza mbele za watu wengine na kuna wengine ni
kujidharau tu na kuona taarifa walizo nazo hazina maana.
Jaribu kuwa na tabia ya kusoma vitu vipya na kuwaeleza watu wengine
na hapo utafanya uwezo wako wa kusimama au kujitokeza mbele ya watu wengine kuwa mkubwa kwa kuwa kichwani
una kitu cha kuwashirikisha.
4.ONGEZA KUJIKUBALI
Ukiwa na tabia ya kujidharau mwenyewe na kujiona huna thamani
mbele ya wengine utafanya aibu ikuteke
daima.
Thamini uwezo wa pekee
ulionao na upe thamani kuwa hakuna mwengine alionao kwahiyo hata wewe
unaweza kuwaonyesha maajabu wasiyoyajua.
Ukijiweka katika kundi
hili hautakuw

No comments:

Post a Comment